Habari

Je wajua: Raisi JK kukamilisha uteuzi wa Bunge la Katiba
Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete, wiki ijayo atakamilisha uteuzi wa majina ya wajumbe 201 wa Bunge Maalumu la Katiba, uteuzi unaoashiria kuanza kwa bunge hilo litakalokuwa na wajumbe 640.
Bunge hilo litakaloanza mwanzoni mwa mwezi ujao mjini Dodoma, litakuwa na kazi ya kuijadili na kuipitisha Rasimu ya Katiba iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Desemba 30 mwaka jana.
Wajumbe wengine watakaounda Bunge hilo ni 42 kutoka vyama vya siasa, 358 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na 81 kutoka Baraza la Wawakilishi.
Januari 2 mwaka huu, ilikuwa siku ya mwisho kwa Ikulu kupokea majina ya makundi mbalimbali ya kijamii ambayo yaliwasilisha mapendekezo ya majina ya watu ambao wangependa wawe wajumbe wa Bunge hilo. Makundi zaidi ya 50 yaliwasilisha majina yao.
Makundi hayo ni asasi za kiraia, mashirika yasiyo ya Serikali, vyama vya kitaaluma, madhehebu ya dini na vyama vya siasa.
Kuanza kwa Bunge hilo kunatarajiwa kuwa na mvutano mkali kutokana na msimamo wa baadhi ya makundi hayo, hasa vyama vya siasa ambavyo vimekuwa vikipingana zaidi katika mfumo wa Serikali tatu uliopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue, ilisema.......

No comments:

Post a Comment